Miaka 52 ya Mapinduzi

Miaka 52 ya Mapinduzi Zanzibar

 WAZANZIBARI  wamesherehekea miaka 52 ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964, ambayo yaling’oa utawala wa Sultani kutoka Oman na kuwezesha wazalendo wengi kushika hatamu ya kuongoza nchi.

Katika kilele cha sherehe hizi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein atahutubia taifa katika uwanja wa Amaan.

Matukio mengine makubwa yaliyofanyika katika uwanja huu ni Rais Shein kukagua gwaride la heshima la vikosi ya ulinzi na usalama, vikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Amepokea maandamano ya wananchi wa mikoa mitano ya Unguja.

Rais John Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu na Viongozi wastaafu, Mzee Mwinyi, Benjamin Mkapa Aman Karume na Wengine Wengi wa Kitaifa, wamewasili uwanja wa Amani katika sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi ya Z'bar.

Vilevile Mkuu wa Majeshi Mwamnyange amehudhulia. Viongozi wengi wa Kitaifa wamehudhulia.

 

 



Post a Comment

Previous Post Next Post