Monday, October 17, 2016
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WA CHUO CHA MAJI UBUNGO WALIOPATA MKOPO 2016/2017
Names of WTF Loan Beneficiaries 2016-17
ATTENTION TO THE WTF LOAN APPLICANTS
The Board of The Registered Trustees of Water Technicians Fund (RTWTF) hereby wishes to inform all loan applicants that by applying and meeting the loan allocation criteria, eighty eight (88) applicants have qualified to be beneficiaries of the loan
for the academic year 2016/2017. The Board likewise disqualified some of the applicants for not adhering to the instructions laid in the form as well as not putting either valid certificates or the required attachments. The board went further to verify the information provided by applicants. The list of successful applicants can be viewed on this website under Publications.
The Board of The Registered Trustees of Water Technicians Fund (RTWTF) hereby wishes to inform all loan applicants that by applying and meeting the loan allocation criteria, eighty eight (88) applicants have qualified to be beneficiaries of the loan
for the academic year 2016/2017. The Board likewise disqualified some of the applicants for not adhering to the instructions laid in the form as well as not putting either valid certificates or the required attachments. The board went further to verify the information provided by applicants. The list of successful applicants can be viewed on this website under Publications.
kuona majina hayo bonyeza hapa
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO MWAKA WA MASOMO 2016/2017-FIRST BATCH
Bodi ya mikopo ya elimu ya juu wametangaza majina ya wanafunzi waliopata mkopo 2016/2017 awamu ya kwanza.
kuona Majina hayo bonyeza hapa
Majina ya mikopo First Batch
kuona Majina hayo bonyeza hapa
Majina ya mikopo First Batch
Tuesday, October 11, 2016
Saturday, October 01, 2016
Monday, September 26, 2016
Haya hapa majina ya udom
The University of Dodoma (UDOM) wishes to announce the names of candidates selected for admission into various undergraduate programmes for the academic year 2016/17.
Admission letters for successful candidates are will be available soon.
to download click here:
SELECTED-CANDIDATES-TO-JOIN-VARIOUS-UNDERGRADUATE-DEGREE-PROGRAMMES-FOR-ACADEMIC-YEAR-2016.2017
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU MWALIMU NYERERE 2016/2017
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU MWALIMU NYERERE 2016/2017
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU TUMAINI MAKUMIRA UNIVERSITY 2016/2017
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA CHUO KIKUU TUMAINI MAKUMIRA UNIVERSITY 2016/2017
makumira-tcu-selection-2016-2017
makumira-tcu-selection-2016-2017
Undergraduate Admission degree Programme 2016/2017
Undergraduate Admission degree Programme 2016/2017
The following applicants have been selected to join various undergraduate degree programmes for the 2016/2017 academic year. The selected applicants should report at the Mwl. J.K. Nyerere Mlimani Campus on Saturday 8th October 2016 for the orientation week which will start on Monday 10th October 2016. Applicants selected for admission into Dar es Salaam University College of Education (DUCE) and Mkwawa University College of Education (MUCE) should report directly to the college's campuses in Chang'ombe and Iringa respectively on the same dates. Joining instructions and admission letters should be collected at the University campuses where one is admitted. Joining instructions and other important information can also be downloaded from the University website
Udsm
Udsm admission 2015/2016
Thursday, September 22, 2016
Sunday, September 18, 2016
Serikali kutoa ubani kwa wafiwa wa tetemeko Bukoba
SERIKALI imesema itatoa fidia ya Sh milioni 1.17 kwa kila familia
iliyofiwa na ndugu wakati wa tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10,
mwaka huu mkoani Kagera.
Taarifa hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akisoma hotuba ya kuahirisha mkutano wa nne wa Bunge la 11.
“Kama Bunge lako tukufu lilivyojulishwa, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imechukua hatua kadhaa kushughulikia athari za tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
“Pamoja na viongozi kutembelea maeneo yenye madhara, Serikali pia imewapatia chakula waathirika, imeimarisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwa kupeleka dawa na vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa na pia imepeleka timu ya wataalamu na madaktari 12 kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando.
“Wananchi waliokosa kabisa hifadhi ya makazi, wamepewa maturubai na mahema kwa ajili ya makazi ya muda na waathirika ambao nyumba zao zimebomoka kabisa kwa kuanzia kila mmoja ametengewa mabati 20, saruji mifuko mitano pamoja na mablanketi na mikeka na kwa wapangaji waliokuwa katika nyumba hizo kila mmoja ametengewa kodi ya pango ya miezi sita ili apate mahali pa kujihifadhi.
“Tathmini ya uharibifu wa barabara imefanyika na barabara zilizoharibika zitarejeshwa katika hali yake ya kawaida ili wananchi waendelee kupata huduma za msingi huku Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kukarabati miundombinu ya maji safi na maji taka.
“Pamoja na hayo, Serikali imewafariji wafiwa na kushiriki mazishi kwa kusaidia kutoa majeneza, sanda, usafiri na kutenga shilingi milioni 20 za rambirambi kwa wafiwa ambazo zitatolewa kwao muda wowote,” alisema Majaliwa.
Pia alizungumzia mwenendo wa ukusanyaji wa mapato serikalini na kusema Serikali imedhamiria kuongeza na kuimarisha ukusanyaji huo kwa kuchukua hatua mbalimbali.
Katika hatua nyingine, alisema katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, mapato ya Serikali yanatarajia kuongezeka na kupunguza utegemezi wa kibajeti kutoka kwa washirika wa maendeleo huku ikiendelea kudhibiti utoaji wa misamaha ya kodi ili kuleta tija kwa Taifa.
“Katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, Serikali imelenga kukusanya mapato ya ndani ikijumuisha mapato ya halmashauri ya jumla ya shilingi trilioni 18.46. Takwimu za mwenendo wa ukusanyaji wa mapato zinaonyesha kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Agosti, mwaka huu, mapato yaliyokusanywa na TRA yalikuwa shilingi trilioni 2.168 ikilinganishwa na makadirio ya kukusanya shilingi trilioni 2.113,” alisema.
Taarifa hiyo ilitolewa bungeni jana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alipokuwa akisoma hotuba ya kuahirisha mkutano wa nne wa Bunge la 11.
“Kama Bunge lako tukufu lilivyojulishwa, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imechukua hatua kadhaa kushughulikia athari za tetemeko la ardhi lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
“Pamoja na viongozi kutembelea maeneo yenye madhara, Serikali pia imewapatia chakula waathirika, imeimarisha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwa kupeleka dawa na vifaa tiba kupitia Bohari Kuu ya Dawa na pia imepeleka timu ya wataalamu na madaktari 12 kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando.
“Wananchi waliokosa kabisa hifadhi ya makazi, wamepewa maturubai na mahema kwa ajili ya makazi ya muda na waathirika ambao nyumba zao zimebomoka kabisa kwa kuanzia kila mmoja ametengewa mabati 20, saruji mifuko mitano pamoja na mablanketi na mikeka na kwa wapangaji waliokuwa katika nyumba hizo kila mmoja ametengewa kodi ya pango ya miezi sita ili apate mahali pa kujihifadhi.
“Tathmini ya uharibifu wa barabara imefanyika na barabara zilizoharibika zitarejeshwa katika hali yake ya kawaida ili wananchi waendelee kupata huduma za msingi huku Serikali ikiendelea kuchukua hatua za kukarabati miundombinu ya maji safi na maji taka.
“Pamoja na hayo, Serikali imewafariji wafiwa na kushiriki mazishi kwa kusaidia kutoa majeneza, sanda, usafiri na kutenga shilingi milioni 20 za rambirambi kwa wafiwa ambazo zitatolewa kwao muda wowote,” alisema Majaliwa.
Pia alizungumzia mwenendo wa ukusanyaji wa mapato serikalini na kusema Serikali imedhamiria kuongeza na kuimarisha ukusanyaji huo kwa kuchukua hatua mbalimbali.
Katika hatua nyingine, alisema katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, mapato ya Serikali yanatarajia kuongezeka na kupunguza utegemezi wa kibajeti kutoka kwa washirika wa maendeleo huku ikiendelea kudhibiti utoaji wa misamaha ya kodi ili kuleta tija kwa Taifa.
“Katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, Serikali imelenga kukusanya mapato ya ndani ikijumuisha mapato ya halmashauri ya jumla ya shilingi trilioni 18.46. Takwimu za mwenendo wa ukusanyaji wa mapato zinaonyesha kuwa katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Agosti, mwaka huu, mapato yaliyokusanywa na TRA yalikuwa shilingi trilioni 2.168 ikilinganishwa na makadirio ya kukusanya shilingi trilioni 2.113,” alisema.
TCU yashusha viwango kujiunga vyuo vikuu
TUME ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), imetangaza kushusha viwango vya
kujiunga na elimu ya juu (GPA) kwa wahitimu wa ngazi ya stashahada
kutoka 3.5 hadi 3.0.
Bila kueleza sababu ya kufikia uamuzi huo, TCU imesema kushushwa kwa viwango hivyo kumelenga kuruhusu idadi kubwa ya wanafunzi kudahiliwa katika vyuo vikuu mbalimbali nchini, huku vigezo vingine vikisalia kama vilivyokuwa awali.
Pamoja na hilo, TCU pia imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu ili kutoa fursa kwa waombaji wenye sifa kuchagua tena kozi zenye nafasi baada ya zile walizoomba awali kujaa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, Eleuther Mwageni, alisema jumla ya walioomba nafasi katika awamu ya kwanza ni 55,347.
Alisema katika awamu hiyo iliyohusisha wanafunzi kutoka kidato cha sita na wenye vyeti kutoka nje ya nchi jumla ya waliodahiliwa ni 30,731 ambapo kidato cha sita ni 30,529 huku wenye vyeti kutoka nje ya nchi wakiwa ni 202.
Waliokosa nafasi katika awamu ya kwanza ni 24,616 ambapo 24,341 ni wale waliohitimu kidato cha sita na 275 ni wenye vyeti kutoka nje ya nchi.
Alisema katika jumla ya waombaji 55,347 walioomba wenye sifa za kudahiliwa ni 47,203 sawa na asilimia 85.3% waliopata ni 30,731 sawa na asilimia 65% waliokosa ni 16,472 sawa na asilimia 35% na wasiokuwa na sifa ni 8,144.
Mwageni alisema wengi waliokosa ni kutokana na kujaa kwa nafasi katika vyuo walivyoomba ambapo idadi kubwa ya waombaji kupendelea zaidi vyuo hivyo.
“Kwa mfano kozi zote zinazotolewa na Muhimbili na nyingi za Chuo cha Ardhi zimejaa, baadhi ya kozi zimekimbiliwa na waombaji wengi kuliko nafasi zilizopo katika vyuo hivyo,” alisema Mwageni.
Alizitaja kozi nyingine zilizojaa katika vyuo vilivyoombwa na idadi kubwa ya waombaji kuwa ni ualimu, udaktari wa binadamu, ufamasia, sayansi ya uthamini wa ardhi na sheria.
“Kozi ya ualimu katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam ilikuwa na waombaji 15,803 wakati nafasi ni 1,000 tu. Halikadhalika kozi ya sayansi ya uthamini wa ardhi ya Chuo Kikuu Ardhi ilikuwa na waombaji 4,599 wakati nafasi ni 100,” alieleza Mwageni.
Aliongeza kuwa waliokosa nafasi ni kutokana na ushindani uliopo kutokana na uhaba wa nafasi katika kozi hizo huku baadhi ya waombaji wakishindwa kuzingatia sifa linganishi.
“Kwa hali hiyo Tume imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu kwa waombaji wenye sifa ili wapate fursa ya kuchagua tena kozi zenye nafasi,” aliongeza Mwageni.
Mapema Julai mwaka huu, Tume hiyo ilitangaza kuongeza viwango vya kujiunga na elimu ya juu kwa wanafunzi waliohitimu ngazi ya stashahada kutoka GPA 2.7 iliyokuwapo awali hadi 3.5.
Bila kueleza sababu ya kufikia uamuzi huo, TCU imesema kushushwa kwa viwango hivyo kumelenga kuruhusu idadi kubwa ya wanafunzi kudahiliwa katika vyuo vikuu mbalimbali nchini, huku vigezo vingine vikisalia kama vilivyokuwa awali.
Pamoja na hilo, TCU pia imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu ili kutoa fursa kwa waombaji wenye sifa kuchagua tena kozi zenye nafasi baada ya zile walizoomba awali kujaa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, Eleuther Mwageni, alisema jumla ya walioomba nafasi katika awamu ya kwanza ni 55,347.
Alisema katika awamu hiyo iliyohusisha wanafunzi kutoka kidato cha sita na wenye vyeti kutoka nje ya nchi jumla ya waliodahiliwa ni 30,731 ambapo kidato cha sita ni 30,529 huku wenye vyeti kutoka nje ya nchi wakiwa ni 202.
Waliokosa nafasi katika awamu ya kwanza ni 24,616 ambapo 24,341 ni wale waliohitimu kidato cha sita na 275 ni wenye vyeti kutoka nje ya nchi.
Alisema katika jumla ya waombaji 55,347 walioomba wenye sifa za kudahiliwa ni 47,203 sawa na asilimia 85.3% waliopata ni 30,731 sawa na asilimia 65% waliokosa ni 16,472 sawa na asilimia 35% na wasiokuwa na sifa ni 8,144.
Mwageni alisema wengi waliokosa ni kutokana na kujaa kwa nafasi katika vyuo walivyoomba ambapo idadi kubwa ya waombaji kupendelea zaidi vyuo hivyo.
“Kwa mfano kozi zote zinazotolewa na Muhimbili na nyingi za Chuo cha Ardhi zimejaa, baadhi ya kozi zimekimbiliwa na waombaji wengi kuliko nafasi zilizopo katika vyuo hivyo,” alisema Mwageni.
Alizitaja kozi nyingine zilizojaa katika vyuo vilivyoombwa na idadi kubwa ya waombaji kuwa ni ualimu, udaktari wa binadamu, ufamasia, sayansi ya uthamini wa ardhi na sheria.
“Kozi ya ualimu katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam ilikuwa na waombaji 15,803 wakati nafasi ni 1,000 tu. Halikadhalika kozi ya sayansi ya uthamini wa ardhi ya Chuo Kikuu Ardhi ilikuwa na waombaji 4,599 wakati nafasi ni 100,” alieleza Mwageni.
Aliongeza kuwa waliokosa nafasi ni kutokana na ushindani uliopo kutokana na uhaba wa nafasi katika kozi hizo huku baadhi ya waombaji wakishindwa kuzingatia sifa linganishi.
“Kwa hali hiyo Tume imeongeza muda wa udahili kuanzia Septemba 12 hadi 23 mwaka huu kwa waombaji wenye sifa ili wapate fursa ya kuchagua tena kozi zenye nafasi,” aliongeza Mwageni.
Mapema Julai mwaka huu, Tume hiyo ilitangaza kuongeza viwango vya kujiunga na elimu ya juu kwa wanafunzi waliohitimu ngazi ya stashahada kutoka GPA 2.7 iliyokuwapo awali hadi 3.5.
Tuesday, August 02, 2016
Friday, July 15, 2016
Monday, July 04, 2016
Mabasi ya haraka kuanza kutumia gesi
MSIMAMIZI wa Usambazaji Gesi katika Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Ismail Naleja, amesema awamu ya pili ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam yatatumia nishati ya gesi asilia badala ya mafuta jambo litakalosaidia kupunguza gharama. Katika awamu ya pili, mabasi mapya 200 ya mradi huo yanatarajiwa kuingizwa nchini.
Akizungumza katika Maonesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, kuhusu usambazwaji wa gesi katika magari, Naleja alisema hatua hiyo itaongeza idadi ya magari yanayotumia gesi nchini ambapo hivi sasa kuna mabasi 60 yanayotumia gesi na kuwashauri wenye magari kutumia mfumo huo ili kupunguza gharama za uendeshaji.
“Uendeshaji wa gesi utakuwa nafuu jambo linaloweza kufanya hata nauli zake kupungua kwani kilo moja ya gesi inatumika katika umbali unaotumiwa na mafuta ya dizeli lita moja na nusu,” alieleza Naleja.
Alisema kilo moja ya gesi ni Sh 1,500 wakati lita moja na nusu ni Sh 3,000, pia gesi haiharibu mazingira kwa sababu haina kaboni ikilinganishwa na petroli.
Aliongeza kuwa, gharama ya ufungaji wa mfumo wa gesi kwenye gari ni Sh milioni mbili, fedha ambayo inarudi baada ya kupunguza gharama katika matumizi kwa miezi mitano tu.
Mtaalamu huyo alisema matumizi ya gesi katika magari si hatari, kwani gesi inayotumika ni nyepesi kuliko inayotumika majumbani, hivyo ikivuja inasambaa hewani na tatizo likitokea mtungi wa gesi unajifunga.
Naye Msemaji wa Kampuni inayoendesha mabasi ya haraka ya UDART, Sabri Mabrouk alisema ni kweli kuwa awamu ya kwanza ya magari yaendayo haraka hayakuweza kutumia gesi kutokana na shirika hilo kuchelewa kupeleka wazo hilo. Hata hivyo sasa wameshafanya mazungumzo ili mradi wa awamu ya pili utumie gesi ili kupunguza gharama.
Alisema wanatarajia awamu ya pili ya mradi utakuwa na mabasi 200.
Kesi za mafisadi kutozidi miezi 9
JAJI Mkuu, Mohammed Chande Othman, amesema Mahakama Maalumu ya
Uhujumu Uchumi na Ufisadi itaamua kesi kwa muda usiozidi miezi tisa na
kwamba itaanza na majaji 14.
Aidha, wameandaa kozi maalumu kwa majaji 14 watakaofanya kazi katika mahakama hiyo itakayoanza Julai 11 hadi 15, mwaka huu, kwenye Chuo cha Mahakama Lushoto mkoani Tanga, ili kupeana mwongozo juu ya uendeshaji wa mahakama hiyo.
Jaji Mkuu alisema, kesi zitakazoendeshwa katika mahakama hiyo ni zile ambazo upelelezi wake umekamilika ili uamuzi utolewe mapema. Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kupambana na uhalifu huo.
Aliyasema hayo jana wakati alipotembelea Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa, ambayo alisema yamezidi kuwa bora kuliko miaka mingine. Alisema baada ya sheria hiyo ya uhujumu uchumi kupitishwa na Bunge, imekuwa na marekebisho mengi na kuboreshwa kwa kiasi kikubwa.
Jaji Mkuu alisema pia, hatua inayofuata ni Rais kutoa idhini ya sheria hiyo na baadaye kupitishwa kwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali ili ianze kutumika.
Alieleza kuwa baada ya kutangazwa katika Gazeti hilo la Serikali, Jaji anatakiwa kutunga kanuni mbalimbali, mojawapo ikiwa ya kulinda mashahidi kutokana na kuwa sheria hiyo inahusu makosa makubwa na hatari ya ugaidi, rushwa na uhujumu uchumi.
“Tuko mbioni kutunga kanuni hizo na kuhakikisha mashahidi wanalindwa. Jengo la mahakama hii litakuwa katika Chuo cha Sheria karibu na Mlimani City na tayari tumepeleka wasajili watendaji,” alisema.
Mwishoni mwa wiki, Jaji Mkuu huyo alisema kuwa majengo ya mahakama hiyo yatakabidhiwa leo. Kutokana na maelezo yake, Mahakama iko tayari kuendesha divisheni hiyo, baada ya kukabidhiwa majengo hayo.
Alisema wataanza kutoa semina kwa majaji na watumishi wengine wa mahakama hiyo juu ya namna divisheni hiyo itakavyoendesha shughuli zake. Aidha, aliweka wazi kuwa hadi sasa hakuna kesi hata moja iliyokwishatambuliwa kwamba itashughulikiwa na mahakama hiyo.
Aidha, wameandaa kozi maalumu kwa majaji 14 watakaofanya kazi katika mahakama hiyo itakayoanza Julai 11 hadi 15, mwaka huu, kwenye Chuo cha Mahakama Lushoto mkoani Tanga, ili kupeana mwongozo juu ya uendeshaji wa mahakama hiyo.
Jaji Mkuu alisema, kesi zitakazoendeshwa katika mahakama hiyo ni zile ambazo upelelezi wake umekamilika ili uamuzi utolewe mapema. Kwa mujibu wa Jaji Mkuu, dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kupambana na uhalifu huo.
Aliyasema hayo jana wakati alipotembelea Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo katika Barabara ya Kilwa, ambayo alisema yamezidi kuwa bora kuliko miaka mingine. Alisema baada ya sheria hiyo ya uhujumu uchumi kupitishwa na Bunge, imekuwa na marekebisho mengi na kuboreshwa kwa kiasi kikubwa.
Jaji Mkuu alisema pia, hatua inayofuata ni Rais kutoa idhini ya sheria hiyo na baadaye kupitishwa kwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali ili ianze kutumika.
Alieleza kuwa baada ya kutangazwa katika Gazeti hilo la Serikali, Jaji anatakiwa kutunga kanuni mbalimbali, mojawapo ikiwa ya kulinda mashahidi kutokana na kuwa sheria hiyo inahusu makosa makubwa na hatari ya ugaidi, rushwa na uhujumu uchumi.
“Tuko mbioni kutunga kanuni hizo na kuhakikisha mashahidi wanalindwa. Jengo la mahakama hii litakuwa katika Chuo cha Sheria karibu na Mlimani City na tayari tumepeleka wasajili watendaji,” alisema.
Mwishoni mwa wiki, Jaji Mkuu huyo alisema kuwa majengo ya mahakama hiyo yatakabidhiwa leo. Kutokana na maelezo yake, Mahakama iko tayari kuendesha divisheni hiyo, baada ya kukabidhiwa majengo hayo.
Alisema wataanza kutoa semina kwa majaji na watumishi wengine wa mahakama hiyo juu ya namna divisheni hiyo itakavyoendesha shughuli zake. Aidha, aliweka wazi kuwa hadi sasa hakuna kesi hata moja iliyokwishatambuliwa kwamba itashughulikiwa na mahakama hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)




















